Katibu Mtendaji wa TAMFI, Winnie Terry.
Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam
Wakati
Serikali ikiwa na malengo ya kufikia asilimia 95 ya
upatikanaji wa maji nchini ifikapo mwaka 2025, Taasisi ya
Tanzania Association of Microfinance Institutions ( TAMFI ) na
wanachama wake wamekuja na mpango wa kuunga mkono juhudi za
Serikali kwa kutoa mikopo kwa wadau wa maji .
Hayo
yamesemwa jijini Dar es Salaam na Makamu Mwenyekiti wa TAMFI
ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Yetu Microfinance, Altemius
Millinga katika warsha ya Siku moja ya kujadili masula ya maji
iliyowakutanisha TAMFI na Taasisi wanachama wa TAMFI
kutoka Tanzania Bara na Zanzibar pamoja Kampuni ya Water
org.
Amebainisha kuwa ili kuunga juhudi za Serikali ya awamu ya
Sita za upatikanaji wa maji wamejipanga kufanikisha
upatikanaji wa huduma hiyo kwa kutoa mikopo kwa ajili ya
huduma za upatikanaji wa huduma ya maji safi na maji taka
kwenye kila kaya yenye uhitaji.
Kwa
upande wake Katibu Mtendaji wa TAMFI, Winnie Terry amefafanua
kuwa katika kufanikisha upatikanaji wa maji wamejipanga
kutoa elimu na kuratibu warsha na mafunzo mbalimbali na
kusaidia taasisi ndogo za kifedha ili waweze kutoa mikopo
inayohusiana na maji na maji taka .
Takwimu
hapa nchini zinaonyesha kuwa upatikaji wa maji vijijini upo
kwa asilimia 70 huku mijini ikiwa ni asilima 85.
Amesisitiza
kuwa mpango huo ni wa miaka mitatu na kwamba TAMFI inalenga kuzisaidia
taasisi za kifedha kwa kuzipa mikopo itakayokwenda kutatua changamoto za
sekta ya maji nchini.
Nae
Mwakilishi wa Taasisi isiyokuwa ya Kiserikali ya Water.org nchini,
Upendo Massawe amesema kuwa wanafanya kazi kwa ukaribu na TAMFI na
kwamba walianza na programu ya kujua tafiti za maji na choo.


%20katika%20Mkutano%20uliojadili%20masuala%20ya%20maji%20uliofanyika%20jijini%20Dar%20es%20Salaam..jpg)


No comments:
Post a Comment