Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi , Vijana Ajira na Watu Wenye Ulemavu
Profesa Joyce Ndalichako amezitaka Taasisi zinazohusika na utoaji wa
Mafao kwa Wastaafu kuacha Urasimu pindi wanapohitaji huduma ya kulipwa
mafao yao.
Ameyasema
hayo jijni Dar es Salaam katika Kongamano na Wazee Wastaafu Mfuko wa
Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) na PSSSF na kwamba kumekuwepo na
changamoto mbalimbali ikiwemo ya mapunjo ya mafao na kuwataka wakuu wa
taasisi hizo kurekebisha kasoro hiyo.
"Mtu
anapokuja hapa lazima aje na vielelezo vya mshahara na nyaraka nyingine
za muhimu lakini kumekuwepo na urasimu usiokuwa wa lazima hivyo
kusababisha usumbufu '" amesema Profesa Ndalichako.
Amebainisha
kuwa kumekuwepo na baadhi ya Taasisi za Umma ambazo haziwasilishi
michango ya wafanyakazi wao hivyo zitachukuliwa hatua kwa mujibu wa
sheria.
Ameongeza
kuwa zipo pia baadhi ya taasisi binafsi ambazo haziwasilishi taarifa za
mafao na kwamba zitabanwa kwa mujibu wa sheria.
Amewataka
watendaji wa mifuko hiyo ya hifadhi ya jamii kuwaondolea ukuta wananchi
wanapokwenda kutaka huduma ikiwemo ikiwemo kuonana na watendaji wakuu
kwa ajili ya kuelezea malalamiko yao juu mafao yao kuwa madogo.
Pia,
amesema kuwa vikao vya kujadili changamoto na kutatua changamoto za
wastaafu vitakuwa endelevu ili kuhakikisha wanapata stahiki zao kwa
wakati mwafaka.
Kwa
upande wake,Chiku Said ambae ni miongoni mwa wastaafu waliofika katika
kikao hicho cha kupeleka malalamiko kuhusu mafao amesema amefanya kazi
na Wizara ya Afya tangu 1973 na kustaafu mwaka 2014 hadi kufikia leo
Julai 22, mwaka 2022 hajapata mafao yake licha ya kufuatilia mara
kadhaa.





No comments:
Post a Comment