HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 19, 2023

  TAIFA GAS yatoa Msaada wa Mitungi ya Gesi 150

Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam

Kampuni ya Usambazaji wa Gesi Majumbani ya Taifa Gas imetoa msaada wa mitungi ya gesi 150 kwa Baba na Mama Lishe wa Kisutu jijini Dar es Salaam.
 
Akizungumza jijini humo wakati wa hafla ya kukabidhi kwa mitungi hiyo Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ngw’ilabuzu Ludigija amempongeza Mbunge wa Jimbo la Ilala ambaye pia ni Naibu Spika Mussa Zungu kwa kushitikiana na Taifa GAS kutoa msaada huo.

“Hongereni kwa kazi nzuri ya kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan za kuhimiza matumizi ya nishati mbadala, hivyo mama lishe na baba lishe haya ni matunda ya maelekezo ya Rais,” amesema Ludigija na kuongeza,

“Hivyo nyie ndiyo wakwanza kula matunda haya ya kuwekwa pamoja mahali rasmi pa kufanyia shughuli zenu,”.

Hivyo Ludigija amewataka baba na mama lishe hao kuwa mabalozi kwa wemgine kuwaeleza kiacha kipikia barabarani kwani kufanya hivyo kuna haribu miundombinu ya barabara.

Ametumia fursa hiyo kuwataka wana Ilala kuhakikisha wanaitikia witu wakufanya shughuli zao katika maeneo rasmi.

Akizungumzia gesi hiyo, amesema kwamba ni salama na itawasaidia kiwaondolea matatizo mbalimbali yakiwemo ya kiafya na mazingira.

Ameelza kwamba Taifa GAS kwa sasa imesambaa nchi nzima, hivyo ameipongeza kampuni hiyo kwa kuunga mkono juhudi za Rais Samia za kuhimiza matumizi ya nishati mbadala ambayo inasaidia kuepusha Taifa kuingia katika hali ya jangwa.

Kwani jambo hilo litasaidia kuokoa misitu kukatwa kwa matumizi ya kuni na mkaa.

Kwa upande wake, Naibu Spika Zungu, amesema kwamba wamesaidia mitungi hiyo kwa sababu baba na mama lishe wamekuwa wakihangaika na moshi kutokana na kutumia mkaa na kuni.

Aidha amesema kwamba baada ya kukaa nao hivi karibuni waliona ni bora kuwasaidia ili waweze kutumia nishati mbadala badala ya mkaa na kuni. 

Naibu Spika Zungu amesema kwamba kutokana na matumizi ya nishati ya kuni na mkaa, takribani viwanja milioni moja vya mpira vyenye misitu vimekuwa vikiharibiwa hali inayosababisha nchi kuingia katika jangwa.

“Tumekaa na Taifa GAS kuwaomba, hivyo mitungi hii 150 inatolewa bure, lakini sharti yake gesi ikiisha utanunua kwa yule aliyekupatia, ukinunua kwingine sio uungwana,” amesema Zungu.

Zungu amewataka kutokuendelea kutumia mkaa na kuni kwani kutumia nishati hizo ni kuliumiza Taifa kwa kuliingiza kwenye ukame.

Nae, Meneja wa Mahusiano Mema kutoka Taifa GAS, Angel Mwita, amesema wametoa msaada wa mitungi hiyo kwa kushirikiana na Mbunge wa Ilala ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Rais Samia za kuhimiza matumizi ya nishati mbadala.

Amesema gesi hiyo ni salama kwa matumizi kwani inasaidia katika utunzaji wa mazingira na kwamba wana gesi ya kutosha kwa matumizi ya nchi nzima

No comments:

Post a Comment

Pages