BAADA ya kufanya vizuri na kazi yake ya ‘Salamu
zao’, msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini, Emmanuel Elibarik ‘Ney wa
Mitego’, anajipanga kusambaza kazi yake mpya inayojulikana kwa jina la ‘Nakula
ujana’.
Mbali na kazi hizo, msanii huyo alishawahi
kutamba na kazi zake nyingine kama, ‘Nasema nao’, ‘Haipotei’ na nyinginezo
ambazo zilimtambulisha na kufanya vizuri katika tasnia ya muziki huo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Ney
alisema wimbo huo ameutoa maalumu kwa wale wote ambao wanasema yeye
anabahatisha katika nyimbo zake, kazi hiyo inaujumbe wa kutosha ndani yake.
“Wengi wameongea sana katika baadhi ya nyimbo zangu, mimi nataka kuwambia kama
mimi sibahatishi nipo kikazi zaidi, ‘Muziki gani’ wanasema Diamond ndio
kanisaidia sijui katika ‘Salamu zao’ nani kanisaidia wao watabaki na maswali
mimi ndio napiga hatua hivyo,” alisema.
Alisema katika wimbo huo kutakua na vitu tofauti
ambavyo havijawahi kuwepo katika uimbaji wake hivyo anaamini uwepo wa mamjonjo
hayo yatasaidia kuipaisha kazi hiyo, na kwamba hapendi kukaa kipindi kirefu
bila kutoa kazi yeyote.
No comments:
Post a Comment