HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 19, 2014

Azam Media wamwaga fedha VPL

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Silas Mwakibinga (kulia), akipokea hundi ya sh. milioni 423.5 kutoka Mtendaji Mkuu wa Azam Media, Rhys Torrington kwa ajili ya klabu zinazoshiriki Ligi Kuu ya Soka Tanzania.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
 
KAMPUNI ya Azam Media Ltd inayomiliki Haki za Matangazo ya Televisheni kwa mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), jana imeikabidhi Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPL Board), kiasi cha shilingi milioni 423.5 ambazo ni za awamu ya pili ya msimu huu wa 2014/15.

Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jengo la Golden Jubilee jijini Dar es Salaam, ambapo kila klabu ya Ligi Kuu imeingiziwa katika akaunti yake mgawo wa shilingi milioni 27.5, kwa ajili ya kusaidia maandalizi ya mwisho na masuala tofauti ya ushiriki.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano hayo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPL Board, Silas Mwakibinga, alizitaka klabu zote za Ligi Kuu ya Vodacom kuhakikisha inazitumia pesa hizo kwa malengo yaliyokusudiwa, ili kuimarisha ushindani katika na kukuza kiwango cha kila timu.

Azam Media Ltd inayomiliki kituo cha televisheni cha Azam Tv, ilitangazwa mshindi wa zabuni za haki ya matangazo ya televisheni kwa mechi za VPL, ambako katika awamu ya kwanza ya pesa hiyo msimu huu iliyotoka Juni 1, mwaka huu, TPL Board ilipokea kitita cha shilingi mil. 462, ambako kila klabu ilijibebea kiasi cha shilingi mil. 25. 

Kwa mujibu wa Mwakibinga, tofauti na msimu uliopita, ambako kila klabu ilipata kitita cha shilingi mil. 100 zilizotolewa katika awamu nne, msimu huu kila klabu itajinyakulia kitita cha shilingi milioni 110, kwa awamu zote nne (sawa na shilingi milioni 27.5 kila awamu).

Kwa upande wake, Mtedaji Mkuu wa Azam Media, Rhys Torrington, alizitakia kila la kheri klabu shiriki katika Ligi Kuu na kwamba kituo chake kiko katika maboresho makubwa ya muonekano wa mechi zitakazorushwa na Azam Tv One na Azam Tv Two, zikiwamo mechi za usiku Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

No comments:

Post a Comment

Pages