HABARI MSETO (HEADER)


 


Breaking

November 07, 2018

WASHINDI WATANO JIDABO NA I&M BANK WATANGAZWA

Mkuu wa Kitengo cha Wateja wa Rejareja wa Benki ya I&M, Ndabu Swere, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, wakati wa kutangaza washindi wa droo ya kwanza ya ‘Jidabo na I&M Bank’ iliyoanza Oktoba 1 hadi Desemba 31. (Picha na Francis Dande).
Mkuu wa Kitengo cha Wateja wa Rejareja wa Benki ya I&M, Ndabu Swere.





Baadhi ya Maofisa wa I&M Bank.
  Washindi wakitangazwa.

NA MWANDISHI WETU


HATIMAYE washindi watano wa Promosheni ya ‘JIDABO na I&M Bank,’ wamepatikana baada ya droo ya kwanza ya shindano hilo kuchezeshwa chini ya wasimamizi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania (GBT). 

‘JIDABO na I&M Bank’, ni promosheni inayoendeshwa na I&M Bank, ambayo inawawezesha wateja wenye akaunti yenye akiba inayoanzia Sh. 200,000, huweza kujishindia kiasi cha pesa mara mbili ya akiba yake isiyozidi Sh. Milioni 5.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa Kitengo cha Wateja wa Rejareja wa I&M Bank, Ndabu Lilian Swere, alisema washindi watano waliopatikana jana ni sehemu ya washindi 15 ambao watapatikana katika kipindi chote cha miezi 3 ya ‘JIDABO na I&M.’ 

“IIi kushiriki JIDABO na Bank I&M, unapaswa kufungua Akaunti ya Akiba, Akaunti ya Biashara, Akaunti ya Mshahara au Akaunti ya Mtoto katika tawi lolote la benki yetu kuanzia Oktoba Mosi mwaka huu hadi Desemba 31,” alisema Swere. 

Aliongeza kuwa, kwa mteja ambaye tayari ana akaunti ya Benki ya I&M, anapaswa kuhakikisha kuwa ana akiba ya Tsh. 200,000, ikiwa anamiliki Akaunti ya Biashara (Current Account) au Tsh. 100,000 ikiwa anamiliki akaunti nyingine zinazohusika katika promosheni. 

Washindi watano waliopatikana katika droo hiyo ya kwanza ya ‘JIDABO na I&M Bank,’ iliyosimamiwa na Chiku Saleh kutoka GBT ni Selcom Wireless Ltd, Jumanne Francis Mchench, Eliakunda Emmanuel Shoo, Sherbanu Osman na Eco Dry Cleaners Ltd.

Kwa mujibu wa promosheni hiyo, washindi hao watano watapata mara mbili ya akiba zilizopo kwenye akaunti zao, ambapo kiwango cha juu zaidi kutolewa kwa mteja kitakuwa Sh. 5,000,000/=. 

Swere alifafanua ya kwamba, ikiwa akiba ya mwezi husika ya mteja ni Sh. Mil. 5, basi itazidishwa mara mbili na kuwa Sh. Mil. 10, na kwamba endapo akiba ya mwezi ya mteja ikizidishwa mara mbili ya kiasi ambacho anatakiwa kuongezewa mteja ili kufika mara mbili ya akiba yake kitazidi Sh. Mil. 5, basi mteja atapewa Sh. Mil. 5 na si zaidi ya hapo. 

“Tunawakaribisha Watanzania wote kuchangamkia fursa hii na kufungua akaunti katika matawi yetu kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Arusha na Moshi Mkoani Kilimanjaro, ili waweze kujidabo na Benki ya I&M na kufanikisha mipango yao mbalimbali iliyobaki kuelekea mwisho wa mwaka 2018,” alimaliza Swere.

No comments:

Post a Comment

Pages