HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 23, 2019

Serikali, Kuboresha Zaidi Mazingira ya Biashara na Uwekezaji Nchini, Na Kuipongeza TradeMark East Africa, Kuunga Mkono Juhudi Hizo

Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai (kushoto), Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Joseph Kakunda, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), George Mkuchika na Naibu wake, Dk. Mary Mwanjwelwa, wakisikiliza mada ya  Mkurugenzi Mkazi wa TradeMark tawi la Tanzania, John Ulanga, kwenye semina ya wabunge wanachama wa Chama cha Wabunge Wanaopambana Rushwa (APNAC) walipokuwa wakijadili kuhusiana na maendeleo ya biashara nchini, iliyofanyika jijini Dodoma hivi karibuni. (Na Mpiga Picha Wetu).


Dodoma, Tanzania

Serikali ya Tanzania Awamu ya Tano chini ya Dk. John Pombe Joseph Magufuli, imedhamiria kwa dhati, kuendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini na mazingira ya  kufanya biashara Tanzania, hivyo kuipongeza Taasisi ya Trade Mark East Africa (TMEA),  kwa kufadhili miradi ya kuboresha biashara kwa ujenzi wa miundombinu ya kisasa na ufadhili wake katika miradi ujenzi wa mifumo ya kidigitali ya kufanya biashara, hivyo kuongeza ushindani wa Tanzania katika kufanya biashara kwa nchi za Afrika Mashariki na Kimataifa.

Pongezi hizo, zimetolewa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Joseph Kakunda,  katika semina ya  Wabunge Kuhusu Fursa za Biashara Ukanda wa Afrika Mashariki,  liyofanyika jana, katika Ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma na ambapo  TradeMark  East Afrika, iliwasilisha Mada ya Mchango wake katika Kuboresha Mazingira ya Biashara nchini, Tanzania.
Waziri Kakunda, amesema Trade Mark East Africa, wanafanya kazi nzuri sana  kuisaidia serikali, ujenzi wa miundombinu ya kisasa na kuboresha mifumo ya kiundeji kuboresha kufanya biashara, biashara ikiwa nzuri, uchumi utakuwa mzuri na TRA itakusanya kodi zaidi na kuleta maendeleo kwa taifa.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejment ya Utumishi wa Umma, Mhe. George Mkuchika, amesema semina hiyo ya TradeMark kwa Wabunge, imewafungua macho kuhusiana na vikwazo vya kisera, kimiondombinu na kisheria vinavyokwamisha biashara, hivyo Wabunge kama watunga sheria, ni muhimu wakavielewa ili kushinikiza mabadiliko ya sheria, taratibu na kanuni za kuodoa vikwazo vyote vya kibiashara na kuifanya Tanzania, kuwa ni nchi kivutio kwa uwekezaji na kufanya biashara.
Kwa upande wake , Mkurugenzi Mkaazi wa TradeMark East Africa, Tawi la Tanzania, John Ulanga, amesema Tanzania ndio nchi yenye fursa kubwa zaidi kibiashara kuliko nchi nyingine zote, kufuatia kupakana na nchi 6 ambazo hazina bahari, hivyo Tanzania ina fursa ya kuwa nchi kitovu cha Biashara kwa nchi za Afrika Mashariki.
Semina hiyo pia ilipokea mada  mchango wa TradeMark East Africa kutoka TRA, TFDA, TPA na Wizara mbalimbali.

No comments:

Post a Comment

Pages