HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 04, 2019

Bashungwa: Kongamano la Tanzania, Uganda liwe chachu ya biashara

NA SALEIMAN MSUYA

WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa amewaoamba wafanyabiashara wa Kitanzania kushiriki katika Kongamano la Kwanza la Biashara na Uwekezaji ili kukuza biashara baina ya nchi hizo.

Kongamano hilo na maonesho ya bidhaa na huduma lifunguliwa na Rais John Magufuli na Rais Yoweri Museven Septemba 6 mwaka huu katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere.

Alisema wafanyabiashara wa Tanzania wanapaswa kutumia fursa zilizopo nchini  ili kuwavutia wenzao wa Uganda.

"Kongamano hili linaloshirikisha wafanyabiashara wa Tanzania na Uganda ni la kwanza kufanyika nawaomba wafanyabiashara na wananchi wajitokeze kwa kujisajili," alisema.

Waziri Bashungwa alisema Tanzania imekuwa ikiuza bidhaa mbalimbali za mazao na vifaa nchini Uganda hivyo kuwataka Watanzania kujitokeza kwa wingi.

"Hii ni fursa kwetu Watanzania tunapaswa kuitumia ili kuweza kunufaika nayo kibishara na kiuchumi," alisema.

No comments:

Post a Comment

Pages