HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 08, 2019

WASAIDIZI WA OFISI CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM WAPIGWA MSASA

Kurugenzi ya Huduma kwa Umma kupitia kitengo cha Mafunzo Endelevu kimetoa mafunzo ya siku nne kwa wasaidizi wa ofisi kuanzia tarehe 8 hadi 11 Oktoba, 2019.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi Huduma kwa Umma Dk. Arnold Towo amesema, “wasaidizi wa ofisi hawana budi kufahamu haki na wajibu wa kazi zao kwa kuzingatia kanuni za Utumishi wa Umma”.
“Kama wasaidizi wa ofisi ni vema kuzingatia maadili ya Utumishi wa Umma muwapo kazini, kufahamu namna bora za utoaji wa huduma kwa mteja pamoja na utunzaji wa kumbukumbu na kutunza siri za ofisi”, alisema Dr. Towo.
Pamoja na hayo Dr. Towo aliwasisitiza wasaidizi wa Ofisi kuzingatia Utunzaji wa muda, mali na usalama wa vitu vya ofisi kwa umakini wanapokuwa sehemu zaoza kazi.
Miongoni mwa masuala ya kuzingatia kazini ni kufanyakazi kwa ushirikiano, kutoruhusu migogoro ambayo husababisha msongo wa mawazo, alisema Dr. Towo.
Mafunzo hayo ya wasaidizi wa Ofisi ni kwa ajili ya kuwajengea uwezo na kuwaongezea ujuzi kazini. Mafunzo hayo yatafungwa rasmi tarehe 11 Oktoba, 2019. 

Imetolewa na Afisa Uhusiano
Kurugenzi ya Huduma kwa Umma
Tarehe 8 Oktoba,2019
Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Huduma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Zamda Kiula, akizungumza na washiriki kabla ya kuanza kwa mafunzo hayo.
Kaimu Mkurugenzi Kurugenzi ya Huduma kwa Umma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dk. Arnold Towo, akifungua mafunzo ya siku nne kwa wasaidizi wa ofisi kuanzia tarehe 8 hadi 11 Oktoba, 2019.
Kaimu Mkurugenzi Kurugenzi ya Huduma kwa Umma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dk. Arnold Towo, akifungua mafunzo ya siku nne kwa wasaidizi wa ofisi kuanzia tarehe 8 hadi 11 Oktoba, 2019.
Baadhi ya washiriki wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa.
Baadhi ya washiriki wakiwa katika mafunzo.
Kaimu Mkurugenzi Kurugenzi ya Huduma kwa Umma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dk. Arnold Towo, akifungua mafunzo ya siku nne kwa wasaidizi wa ofisi kuanzia tarehe 8 hadi 11 Oktoba, 2019.
Mtumishi kutoka Kituo cha Afya, Anna Mwahu, akijitambulisha kabla ya kuanza kwa mafunzo.
Utambulisho.
Shaban Msumi kutoka Ofisi ya Makamu Mkuu wa Chuo akichangia mada katika mafunzo hayo.
Mshiriki.
Mkufunzi wa Mafunzo ya Wasaidizi wa Ofisi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Peter Mbago, akitoa mada kuhusu Huduma kwa Wateja.
Washiriki.
Washiriki.



Washiriki wakichangia mada.
Mtumishi kutoka Ndaki ya Sayansi ya Jamii, Said Matimbwa.
Shaban Msumi kutoka Ofisi ya Makamu Mkuu wa Chuo.

No comments:

Post a Comment

Pages