HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 14, 2025

MBUNGE MTEULE JASMINE NG'UMBI KUWAPIGANIA VIJANA BUNGENI

NA DENIS MLOWE, IRINGA 

MBUNGE Mteule wa Viti Maalum Vijana Taifa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka mkoa wa Iringa, Jasmine Ng’umbi, ameahidi kutumia nafasi yake bungeni kuhamasisha na kusukuma mbele miradi inayowagusa moja kwa moja vijana na wanawake, ili kuongeza fursa za maendeleo kwa makundi hayo.

Akizungumza leo wakati Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Stephen Wasira, akizindua kampeni za wagombea ubunge na udiwani katika majimbo ya Kalenga na Iringa Mjini, Jasmine alisema anaingia bungeni akiwa na azma ya kuhakikisha vijana na wanawake wanapata nafasi kubwa zaidi kiuchumi na kijamii.

Jasmine pia aliwataka wananchi wa Iringa na Watanzania kwa ujumla kuhakikisha wanampa kura za kishindo Dk Samia, wabunge na madiwani, akisema chama hicho kimeonesha kwa vitendo kwamba kina uwezo wa kusukuma maendeleo kwa wote bila ubaguzi.

“Rais Samia ameonesha mfano wa uongozi wa vitendo. Sasa ni jukumu letu kuendeleza kasi hiyo kwa kuhakikisha CCM inaendelea kupewa ridhaa ya kuongoza, ili vijana, wanawake na Taifa kwa ujumla waendelee kufaidika,” alisisitiza.

 

No comments:

Post a Comment

Pages